Thursday, February 7, 2013

ASKOFU THOMAS LAIZER WA KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI KATI AFARIKI DUNIA


Askofu Thomas Laizer enzi za uhai wake.
HABARI zilizotufikia hivi punde kutoka Jijini Arusha zinaarifu kuwa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati, Askofu Thomas Laizer amefariki dunia.

Taarifa hizo zinadai kuwa Askofu Laizer amefikwa na umauti alasiri ya leo katika Hospitali ya Rufaa ya Selelian ya Mjini Arusha.

Jana Februari 6, 2013 Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alimtembelea  na kumjulia hali Askofu Thomas Laizer wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati.…

Askofu Thomas Laizer enzi za uhai wake.
HABARI zilizotufikia hivi punde kutoka Jijini Arusha zinaarifu kuwa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati, Askofu Thomas Laizer amefariki dunia.
Taarifa hizo zinadai kuwa Askofu Laizer amefikwa na umauti alasiri ya leo katika Hospitali ya Rufaa ya Selelian ya Mjini Arusha.
Jana Februari 6, 2013 Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alimtembelea  na kumjulia hali Askofu Thomas Laizer wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati.
Taarifa zilipasha kuwa Askofu Laizer alilazwa Hospitalini hapo kwa zaidi ya mwezi mmoja, na hakuna daktari wala ndugu aliye tayari kusema ugonjwa unaomsibu.
Pinda alikwenda hospitalini hapo jana saa 9 alasiri na kukaa zaidi ya nusu saa, huku waandishi wa habari wakizuiwa kuingia katika chumba alimolazwa cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu.
Hata hivyo, baada ya kutoka katika chumba hicho kama ilivyo ada ya viongozi kuzungumzia hali ya mgonjwa, Pinda hakuzungumza na waandishi wa habari na kulikuwa na ulinzi mkali ambapo pia waandishi wa habari walizuiwa kuzungumza naye.
Awali ilisemekana kuwa Askofu Laizer amehamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC ya Moshi mkoani Kilimanjaro, baada ya watu wengi kumiminika Selian kutaka kumwona, lakini jana ilidhihirika kuwa, amelazwa hospitalini hapo.
 FK Blog inatoa pole kwa Waumini na washarika wote wa KKKT nchini kote kufuatia msiba huo mzito ulilolikumba Kanisa la Kilutheri hasa wakati huu ambao kuna mgongano kati ya waumini na Viongozi wa Dayosisi ya Kaskazini Kati.

Saturday, December 29, 2012

Watu 8 wafariki nchini Kenya

 29 Disemba, 2012 - Saa 14:25 GMT

Familia zilizoathiriwa
Familia zilizoathiriwa kwa mujibu wa Gazeti la Standard Nchini Kenya wakipekuwa mali yao baada ya maporomoko hayo ya Ardhi
Watu wanane wamekufa baada ya nyumba kadha kufukiwa na maporomoko ya ardhi katika eneo la bonde la Kerio, magharibi mwa Kenya, jana usiku.
Maporomoko ya ardhi yamesababishwa na mvua kubwa zilizonyesha katika bonde hilo. Eneo la Kerio pia limekumbwa na mafuriko kutokana na mvua kubwa inayonyesha.
Chama cha Msalaba Mwekundu cha Kenya kinasaidia jitihada za uokoaji na kutoa taarifa kwamba miili miili ya watu wanane imeonekana na watu wengine watano waliokolewa mapema leo.
Watu wengi hawana makaazi kutokana na nyumba zao kusombwa na maji au kufukiwa na maporomoko ya ardhi.

Friday, October 12, 2012

VURUGU ZA MAANDAMANO YA WAISLAMU MBAGALA KIZUIANI LEO

Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu wakiandamana kupinga kitendo cha kijana Emmanuel Josephat anayedaiwa kukojolea Quran.
Barabara ikiwa imefungwa wakati wa vurugu hizo.
Wananchi wakishuhudia vurugu hizo.
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia wakiwa na baadhi ya watuhumiwa waliokamatwa katika vurugu hizo za maandamano.Wanausalama wakiwa kazini kuzuia vurugu hizo.

Saturday, October 6, 2012

ALICHO KIANDIKA DIAMOND KATIKA WEBSITE YAKE KUHUSIANA NA BRITHDAY YA WEMA SEPETU

Mwaka 1990, mwezi na siku kama ya leo Mrs. Abraham Sepetu ama (Mama Sepetu) alipata bahati ya kujifungua mtoto wa kike ambae alimtunuku jina la Wema Abraham Sepetu, Mtoto ambae Nyota yake ilianza kama masihara tu pale aliposhinda taji la Miss Tanzania 2006, kisha baadae kuingia katika Muvie Industry kama utaniutani vile na ghafla kuwa DIVA wa Tasnia hiyo, na licha tu ya udiva pia kuwa ICON wa Tanzania.Siku hii ya leo ya tarehe 28/09/ anazaliwa upya na kutimiza miaka 22.Honestly nina furaha sana na kila sababu yakusema "Happy Birthday Sepetu wa Sepetunga"....coz kiukweli ni mtu ambae kwa namna moja au nyinge anamchango mkubwa sana katika Mafanikio yangu hadi kufikia hapa nilipo, Sikuzote amekua akinipa Moyo, Motisha,Nguvu na kunisupport kwa hali na mali ili tu niweze kufika Mbali zaidi..toka kwenye "Upenzi" hadi leo kwenye "Cousins" mixer "Ushemlake" ni mbali sana nimetoka nae...narudia tena kusema nina BOOooonge la furaha na kila sababu ya kumwambia "Happy birthday Sepetu wa sepetunga" wish you all the best mama.....Maisha marefu yenye amani na Mafanikio tele..........wote tuseme Aaaamen!

Tuesday, October 2, 2012

THE LEGEND IS BACK


RICK ROSS: ASKARI MAGEREZA ALIYEGEUKA BILIONEA


WAKATI habari ya mjini ikiwa ni ujio wa mkali William Leonard Roberts II ‘Rick Ross’ kunako Tamasha la Serengeti Fiesta Bongo, Oktoba 6, 2012, usilolijua kuhusu mkali huyu ni kwamba aliwahi kuwa askari magereza (Correctional Officer) kwenye Gereza la Florida kwenye miaka ya 1990 kabla ya kugeukia gemu la Hip Hop alikotusua mkwanja wa maana.
Sababu za mkali huyo kutema mzigo wa magereza hazijawekwa wazi ingawa inadaiwa kuwa tatuu alizojichora, rekodi ya makosa ya jinai kama matumizi ya bunduki, kukutwa na kitu cha marijuana na mengineyo, vilisababisha asimamishwe mzigo, akaona isiwe tabu, mwaka 2002 akaingia kwenye Rap Game na kuanza kuchana mistari na kugeuka bilionea.

MAGARI MAWILI YAGONGANA NA KUWAKA MOTO MBALIZI MKOANI MBEYA, 10 WALIPOTIWA KUFARIKI DUNIA, MBUNGE WA VITI MAALUM MARY MWANJELWA ANUSURIKA, KATIBU WAKE ATEKETEA KWA MOTO


 HIVI NDIVYO MAAFA YALIVYO.

 GARI LILIVYO UNGUA MOTO BAADA YA AJALI.


 MAMIA YA WATU WALIOFIKA KUSHUHUDIA AJALI HIYO MBALIZI JIJINI MBEYA.


GARI HILI LILIVYOPINDUKA NA KUWAKA MOTO BAADA YA AJALI.
 MKUU WA MKOA WA MBEYA ALIYEVAA SUTI YA BLUU, MH. ABAS KANDORO AKIWA ENEO LA AJALI.
 HII NI GARI NYINGINE AMBAYO PIA ILIWAKA MOTO BAADA YA KUGONGANA.
 ZIMAMOTO WAKIWA ENEO LA TUKIO KWA AJILI YA KUZIMA MOTO HUO.
 ASKARI WA USALAMA BARABARANI WAKIWA ENEO LA TUKIO AMBAPO AJALI HIYO IMESABABISHA VIFO VYA WATU KUMI.
 WATU WAKIWA WAMEONGEZEKA KUSHUHUDIA TUKIO HILI LA AJALI.
 MUONEKANO WA GARI HILI LIKIWA LIMEUNGUA LOTE.
MABAKI YA GARI HILI AMBALO NALO LILIUNGUA LOTE.
WANANCHI WAKIWA WANASHUHUDIA AJALI HUKU WENGINE WAKIWA WANAENDELEA KUOKOA MAJERUHI WA AJALI HIYO.
KIKOSI CHA FFU NAO WALIKUWEPO SAMBAMBA KATIKA KUHAKIKISHA ZOEZI LA UOKOAJI LINAENDA KIKAMILIFU.
PIA KATIKA ENEO HILI  MBUNGE WA VITI MAALUM MH.MARY MWANJELWA ALIKUWEPO NDANI YA PICK UP ILIYOUNGUA MOTO, KATIBU WAKE AMETEKETEA KWA MOTO NDANI YA GARI HILO.
HABARI KAMILI ITAWAJIA BAADAE.
 TONE MEDIA LIVE GROUP TUMESHUHUDIA TUKIO HILI.