Friday, October 12, 2012

VURUGU ZA MAANDAMANO YA WAISLAMU MBAGALA KIZUIANI LEO

Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu wakiandamana kupinga kitendo cha kijana Emmanuel Josephat anayedaiwa kukojolea Quran.
Barabara ikiwa imefungwa wakati wa vurugu hizo.
Wananchi wakishuhudia vurugu hizo.
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia wakiwa na baadhi ya watuhumiwa waliokamatwa katika vurugu hizo za maandamano.Wanausalama wakiwa kazini kuzuia vurugu hizo.

Saturday, October 6, 2012

ALICHO KIANDIKA DIAMOND KATIKA WEBSITE YAKE KUHUSIANA NA BRITHDAY YA WEMA SEPETU

Mwaka 1990, mwezi na siku kama ya leo Mrs. Abraham Sepetu ama (Mama Sepetu) alipata bahati ya kujifungua mtoto wa kike ambae alimtunuku jina la Wema Abraham Sepetu, Mtoto ambae Nyota yake ilianza kama masihara tu pale aliposhinda taji la Miss Tanzania 2006, kisha baadae kuingia katika Muvie Industry kama utaniutani vile na ghafla kuwa DIVA wa Tasnia hiyo, na licha tu ya udiva pia kuwa ICON wa Tanzania.Siku hii ya leo ya tarehe 28/09/ anazaliwa upya na kutimiza miaka 22.Honestly nina furaha sana na kila sababu yakusema "Happy Birthday Sepetu wa Sepetunga"....coz kiukweli ni mtu ambae kwa namna moja au nyinge anamchango mkubwa sana katika Mafanikio yangu hadi kufikia hapa nilipo, Sikuzote amekua akinipa Moyo, Motisha,Nguvu na kunisupport kwa hali na mali ili tu niweze kufika Mbali zaidi..toka kwenye "Upenzi" hadi leo kwenye "Cousins" mixer "Ushemlake" ni mbali sana nimetoka nae...narudia tena kusema nina BOOooonge la furaha na kila sababu ya kumwambia "Happy birthday Sepetu wa sepetunga" wish you all the best mama.....Maisha marefu yenye amani na Mafanikio tele..........wote tuseme Aaaamen!

Tuesday, October 2, 2012

THE LEGEND IS BACK


RICK ROSS: ASKARI MAGEREZA ALIYEGEUKA BILIONEA


WAKATI habari ya mjini ikiwa ni ujio wa mkali William Leonard Roberts II ‘Rick Ross’ kunako Tamasha la Serengeti Fiesta Bongo, Oktoba 6, 2012, usilolijua kuhusu mkali huyu ni kwamba aliwahi kuwa askari magereza (Correctional Officer) kwenye Gereza la Florida kwenye miaka ya 1990 kabla ya kugeukia gemu la Hip Hop alikotusua mkwanja wa maana.
Sababu za mkali huyo kutema mzigo wa magereza hazijawekwa wazi ingawa inadaiwa kuwa tatuu alizojichora, rekodi ya makosa ya jinai kama matumizi ya bunduki, kukutwa na kitu cha marijuana na mengineyo, vilisababisha asimamishwe mzigo, akaona isiwe tabu, mwaka 2002 akaingia kwenye Rap Game na kuanza kuchana mistari na kugeuka bilionea.

MAGARI MAWILI YAGONGANA NA KUWAKA MOTO MBALIZI MKOANI MBEYA, 10 WALIPOTIWA KUFARIKI DUNIA, MBUNGE WA VITI MAALUM MARY MWANJELWA ANUSURIKA, KATIBU WAKE ATEKETEA KWA MOTO


 HIVI NDIVYO MAAFA YALIVYO.

 GARI LILIVYO UNGUA MOTO BAADA YA AJALI.


 MAMIA YA WATU WALIOFIKA KUSHUHUDIA AJALI HIYO MBALIZI JIJINI MBEYA.


GARI HILI LILIVYOPINDUKA NA KUWAKA MOTO BAADA YA AJALI.
 MKUU WA MKOA WA MBEYA ALIYEVAA SUTI YA BLUU, MH. ABAS KANDORO AKIWA ENEO LA AJALI.
 HII NI GARI NYINGINE AMBAYO PIA ILIWAKA MOTO BAADA YA KUGONGANA.
 ZIMAMOTO WAKIWA ENEO LA TUKIO KWA AJILI YA KUZIMA MOTO HUO.
 ASKARI WA USALAMA BARABARANI WAKIWA ENEO LA TUKIO AMBAPO AJALI HIYO IMESABABISHA VIFO VYA WATU KUMI.
 WATU WAKIWA WAMEONGEZEKA KUSHUHUDIA TUKIO HILI LA AJALI.
 MUONEKANO WA GARI HILI LIKIWA LIMEUNGUA LOTE.
MABAKI YA GARI HILI AMBALO NALO LILIUNGUA LOTE.
WANANCHI WAKIWA WANASHUHUDIA AJALI HUKU WENGINE WAKIWA WANAENDELEA KUOKOA MAJERUHI WA AJALI HIYO.
KIKOSI CHA FFU NAO WALIKUWEPO SAMBAMBA KATIKA KUHAKIKISHA ZOEZI LA UOKOAJI LINAENDA KIKAMILIFU.
PIA KATIKA ENEO HILI  MBUNGE WA VITI MAALUM MH.MARY MWANJELWA ALIKUWEPO NDANI YA PICK UP ILIYOUNGUA MOTO, KATIBU WAKE AMETEKETEA KWA MOTO NDANI YA GARI HILO.
HABARI KAMILI ITAWAJIA BAADAE.
 TONE MEDIA LIVE GROUP TUMESHUHUDIA TUKIO HILI.

TASWIRA ZA BASI LA DAR EXPRESS LIKITEKETEA KWA MOTO LEO ASUBUHI

Basi la Dar Express lililokuwa likitokea Arusha kwenda Dar likiteketea kwa moto eneo la Segera, mkoani Tanga leo asubuhi. Abiria wote 65 wamenusurika.

SUGU ADATA BAADA YA KUPATA MTOTO

UMESHAWAHI kuona mtu mzima amedata? Basi kwa taarifa yako habari za kupata mtoto, zilipomfikia Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, alitulia kama maji mtungini kwa muda, baada ya muda mfupi akaamka na kushangilia kwa nguvu, Showbiz inakumegea.
Kwa watu waliomzoea Sugu, walishangazwa na furaha yake, kwani ‘mudi’ yake ilikuwa juu mno baada ya kusoma SMS ya kumueleza kwamba yeye ni baba wa mtoto wa kike. Waliokuwa karibu yake, walipomuuliza, Sugu alitamka mfululizo: “My daughter, I’m now a father. My daughter, I’m the happiest MP right now.”
Alimaanisha: Binti yangu, sasa mimi ni baba. Binti yangu, sasa mimi ni mbunge mwenye furaha zaidi.
Jumatano iliyopita (Septemba 26, 2012) usiku, Sugu alipokea SMS kutoka kwa mzazi mwenzake, anayekwenda kwa jina la Faiza, asubuhi ya siku iliyofuata, hakuweza kuendelea kukaa Mbeya, alisafiri kwa mkoko wake wa heshima, Toyota Land Cruiser Amazon hadi Dar kumuona binti yake.
Mtoto huyo, Sugu amempa jina la Sasha-Desderia Joseph Mbilinyi. Kama ulikuwa hujafunuliwa, jina la Desderia ni la mama mzazi wa mbunge huyo, anayeitwa Desderia Mbilinyi ‘Mama Mbilinyi’.
Akizungumza na Showbiz, Sugu alisema: “Kwanza namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kumpata Sasha-Desderia. Ni mtoto ambaye amekuja ndani ya mahitaji yangu. Yaani nilimhitaji na kweli amekuja.
“Kwa mama wa mtoto (Faiza), namuomba sana Mungu atujaalie maisha marefu yenye furaha na maelewano, tuweze kumlea mtoto wetu.”
Sasha-Desderia, ni mtoto wa kwanza wa Sugu ambaye mbali na ubunge, jina lake lipo juu kwa takriban miongo miwili sasa kutokana na harakati zake kwenye muziki wa Hip Hop na Bongo Fleva, akiwa ameshatoa albamu 10, pamoja nyimbo zinazobamba zaidi ya 40.

WALIOVUNJA UCHUMBA WA WOLPER HAWA HAPA


Na Mwandishi Wetu
SIYO habari mpya kwamba ule uchumba wa kitajiri kati ya staa wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper Massawe na mfanyabiashara ‘mjanjamjanja’, Abdallah Mtoro ‘Dallas’ umevunjika, kinachotengeneza kichwa cha habari leo ni sababu iliyo nyuma ya kuachana kwao.
Uwazi ‘Mama wa Magazeti Pendwa’, linakuwa la kwanza kuanika sababu ya kuachana kwao, ikiwa ni kutaja majina ya watu ambao wamekuwa sababu ya kumwagana kwao.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, sababu ya kwanza ni Wolper kuwa na hisia mbaya dhidi ya wanawake kadhaa, akiamini kwamba kuna kitu cha zaidi kati yao na Dallas.
Chanzo chetu kikataja majina ya watuhumiwa: “Lulu Mathias Semagongo ‘Aunty Lulu’, Halima Haroun ‘Halima Kimwana Manywele’, Khadija Shaibu ‘Dida’, Mohamed Ndama ‘Mtoto wa Ng’ombe’ na mwanamke mwengine aliyetajwa kwa jina moja la Sabaha.”
Kikafafanua sababu ya kila mmoja kutajwa: “Dida anatajwa kwa sababu moja kuu, kwa muda mrefu amekuwa akitambulika kama dada wa Dallas, kwa hiyo akawa anamwita Wolper wifi. Baadaye Wolper akawa na hisia mbaya na Dida, akaanza maswali.
“Kwa kawaida Dallas ni mtu asiyejali, kwa hiyo akawa anampotezea, yaani hampi majibu yaliyonyooka. Wolper alikuwa anataka kujua Dida ni dada yake Dallas kivipi? Kimjinimjini au ni ndugu kabisa. Wolper alipoona hakuna jibu la kunyooka, akaweka kinyongo, akawa hana imani na Dida.
“Wolper anaamini kwamba Dallas ametembea na Aunty Lulu, Halima Kimwana na Sabaha. Upande wa Ndama, Wolper alishamshtaki Ndama kwa kumtapeli. Sasa hivi Dallas na Ndama wapo pamoja, kwa hiyo Wolper anahisi anasalitiwa na mchumba wake. Mwisho akaona bora waachane.”
Baada ya maelezo hayo kutoka kwa chanzo chetu, mwandishi wetu alizungumza na Wolper ambaye alikiri kuachana na Dallas, alipobanwa kuhusu sababu alikata simu, baadaye akaandika SMS: “Dallas ni mchafu, nimeshamfumania sana. Anatembea na wanawake hovyo.”
Alipopigiwa simu mara ya pili na kutakiwa kutaja majina ya wanawake ambao ameona wamekuwa na uhusiano na Dallas, hakuyaweka wazi ila alisema: “Nikiwazungumzia nitaonekana namuonea wivu, ila kwa kifupi Dallas amenidhalilisha. Ametembea mpaka na wanawake ambao siyo daraja langu kabisa.
“Mimi nilimheshimu Dallas, unajua alipokuwa nje alikuwa ananiheshimu kama mke wake mtarajiwa. Unajua mtu tabia yake utaijua mkiwa pamoja. Sasa aliporudi hapa na vitendo alivyofanya ndiyo nimeamini siyo mtu mzuri, hastahili kuwa mume wangu kabisa.
“Wakati mwingine nimekaa nyumbani, naambiwa Dallas yupo na wanawake. Navaa kininja, nakodi teksi, nikifika nashuhudia kila kitu halafu narudi nyumbani. Nimejionea mengi na mpaka sasa simhitaji tena. Nimeona wanawake zake, siyo hadhi yangu lakini kanichanganya nao.”
Aunty Lulu alipoulizwa alisema, hajawahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Dallas, akaongeza: “Tatizo Dallas anapenda sana utani, unaweza kukaa naye, watu wakija ananitambulisha mimi ni mke wake. Hilo ndiyo tatizo.”
Dida yeye alisema anashangaa kutajwa kwenye sakata la Wolper na Dallas kwa sababu ana zaidi ya miaka saba, hajakutana na mfanyabiashara huyo mjanjamjanja.
Halima Kimwana, Ndama na Dallas hawakupatikana lakini nafasi yao bado ipo ili nao waelezee kilichopo upande wao. Waandishi wetu bado wapo kazini wanawatafuta.