Friday, June 29, 2012

Wageni watekwa wakiwa kambini Kenya


 29 Juni, 2012 - Saa 12:48 GMT
Polisi nchini Kenya wamesema kuwa wafanyikazi sita wa shirika la kutoa misaada kwa wakimbizi wametekwa nyara katika kambi ya wakimbizi ya Ifo ilioko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Dadaab
kambi hiyo inatoa hifadhi wakimbizi nusu milioni
Waliotekwa ni wafanyikazi wa shirika la Norwegian Refugee Council, ambalo linatoa huduma kwa wakimbizi kutoka Somalia wanaoishi kwenye kambi hiyo.
Msemaji wa Shirika hilo, amedhibitisha tukio hilo na kuongeza kuwa katibu mkuu Elizabeth Rasmussen alikuwemo kwenye msafara uliovamiwa lakini amenusurika.
Hata hivyo shirika hilo halijatoa taarifa zaidi kuhusu tukio hilo na watu waliotekwa.
Mkuu wa wilaya ya Lagdera ambako kambi hiyo ipo Robert Kimanthi amesema waliotekwa ni raia wa Canada, Norway, Mfilipino, Mpakistani na Wakenya wawili. Wote ni wanaume.
Kulingana na polisi watu waliokuwa wamejihami kwa bunduki walishambulia msafara wa magari katika kambi hiyo ambayo inatoa makaazi kwa zaidi ya wakimbizi nusu milioni kutoka Somalia. Mtu mmoja aliuawa kwenye tukio hilo.
Polisi wanashuku kuwa wapiganaji wa kiisalamu wa Al shaabab walihusika na shambulio hilo.
Visa vya mashambulio ya kigaidi vimeongezeka katika maeneo ya kaskazini mwa Kenya, baada ya wanajeshi wake kuingia nchini Somalia mwaka jana kupambana na wanamgambo wa al shabaab.
Katika miezi ya hivi karibuni, wafanyakazi kadhaa wa mashirika ya kutoa misaada wametekwa nyara katika kambi hiyo ya Daadab.
Wawili kati yao ni wanawake wawili raia wa uhispania ambao walitekwa nyara mwezi Oktoba mwaka uliopita.

LULU AFUNGUKA ASE BADO NATESEKA






Stori: Richard Bukos
MSANII wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ juzi Jumatatu aliwaambia ndugu zake kuwa bado anateseka baada ya kesi yake inayomkabili ya kuhusishwa na kifo cha msanii mwenzake, Steven Kanumba kupigwa kalenda baada ya suala lake kuhusu umri wake kuamriwa kupelekwa Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Muda mfupi baada ya uamuzi huo uliofikiwa Mahakama Kuu mbele ya Jaji Twalib Fauz anayesikiliza kesi hiyo na Lulu kutolewa katika chumba cha mahakama tayari kwa kurudishwa rumande, msanii huyo aligonganisha macho na mmoja wa ndugu zake huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Bado nateseka,” alisema Lulu bila kuongeza neno lingine hali iliyozua majonzi mazito kwa ndugu yake huyo.
Lulu (pichani) alifikishwa katika Makahama Kuu ya Tanzania ambapo kesi yake ilitajwa tena mbele ya Jaji Fauz kwa lengo la upande wa utetezi kuwasilisha vielelezo vya kuthibitisha umri wake ambapo unadai hajafikisha miaka 18.
UTETEZI WAKWAMA TENA
Hata hivyo, upande wa utetezi ukiwa tayari kuwasilisha vielelezo vyao, Jaji Fauz alimtaka Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda kuzungumza lolote kabla mawakili wa Lulu kutoa vithibitisho vyao kama ushahidi.
Wakili Kaganda aliibua hoja mpya ya kupinga vielelezo hivyo kutolewa mahakamani hapo na kusema wameshapeleka hati ya rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa kupinga kujadili upya umri wa msanii huyo mahakamani hapo.
Awali wakiwa mahakamani hapo, mawakili wa pande zote walifikia muafaka wa kuujalidi upya umri wa msanii huyo ambapo serikali ilipeleka vielelezo vya umri wa Lulu kuwa ni miaka 18.
Hata hivyo, juzi upande huo wa Jamhuri uliomba kusitishwa kwa zoezi hilo baada ya kukata rufaa ili uendelee kutambulika kuwa ni miaka 18 aliouandikisha msanii huyo na kutia saini yake alipokuwa akihojiwa kituo cha polisi baada ya kukamatwa kuhusu kesi hiyo.
Kufuatia ombi hilo hilo la rufaa, mawakili wa Lulu, Kennedy Fungamtama, Peter Kibatala na Fulgency Massawe waliushutumu upande wa Jamhuri kwa kuwasumbua na kuwa vigeugeu kwani wao ndiyo walioomba kesi hiyo itolewe Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kupelekwa mahakamani hapo kwa ajili ya kujadili umri.
Jaji Fauz aliipitia nakala ya barua iliyopelekwa Mahakama ya Rufaa na mawakili wa serikali na kutoa uamuzi kuwa kesi hiyo ipelekwe Mahakama ya Rufaa kwa ajili ya kutolewa upya uamuzi wa kujadili umri wa msanii huyo.

DK. CHENI AWATENGANISHA WAZAZI WAKE
Katika hali ya kushangaza, wazazi wa Lulu, hawakukaa pamoja, msanii wa filamu, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ ndiye aliyekaa katikati yao.
Jambo lililozidisha huzuni mahakamani hapo ni mdogo wake ambaye jina lake halikupatikana mara moja, kupelekwa kumsamilia sehemu aliyokuwa amekaa huku akiwa amezungukwa na maaskari magereza.
Hali hiyo ilimfanya Lulu amwage machozi kwa uchungu.
Kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Julai 09, mwaka huu kabla ya kuhamishiwa Mahakama ya Rufaa.





Stori: Richard Bukos
MSANII wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ juzi Jumatatu aliwaambia ndugu zake kuwa bado anateseka baada ya kesi yake inayomkabili ya kuhusishwa na kifo cha msanii mwenzake, Steven Kanumba kupigwa kalenda baada ya suala lake kuhusu umri wake kuamriwa kupelekwa Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Muda mfupi baada ya uamuzi huo uliofikiwa Mahakama Kuu mbele ya Jaji Twalib Fauz anayesikiliza kesi hiyo na Lulu kutolewa katika chumba cha mahakama tayari kwa kurudishwa rumande, msanii huyo aligonganisha macho na mmoja wa ndugu zake huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Bado nateseka,” alisema Lulu bila kuongeza neno lingine hali iliyozua majonzi mazito kwa ndugu yake huyo.
Lulu (pichani) alifikishwa katika Makahama Kuu ya Tanzania ambapo kesi yake ilitajwa tena mbele ya Jaji Fauz kwa lengo la upande wa utetezi kuwasilisha vielelezo vya kuthibitisha umri wake ambapo unadai hajafikisha miaka 18.
UTETEZI WAKWAMA TENA
Hata hivyo, upande wa utetezi ukiwa tayari kuwasilisha vielelezo vyao, Jaji Fauz alimtaka Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda kuzungumza lolote kabla mawakili wa Lulu kutoa vithibitisho vyao kama ushahidi.
Wakili Kaganda aliibua hoja mpya ya kupinga vielelezo hivyo kutolewa mahakamani hapo na kusema wameshapeleka hati ya rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa kupinga kujadili upya umri wa msanii huyo mahakamani hapo.
Awali wakiwa mahakamani hapo, mawakili wa pande zote walifikia muafaka wa kuujalidi upya umri wa msanii huyo ambapo serikali ilipeleka vielelezo vya umri wa Lulu kuwa ni miaka 18.
Hata hivyo, juzi upande huo wa Jamhuri uliomba kusitishwa kwa zoezi hilo baada ya kukata rufaa ili uendelee kutambulika kuwa ni miaka 18 aliouandikisha msanii huyo na kutia saini yake alipokuwa akihojiwa kituo cha polisi baada ya kukamatwa kuhusu kesi hiyo.
Kufuatia ombi hilo hilo la rufaa, mawakili wa Lulu, Kennedy Fungamtama, Peter Kibatala na Fulgency Massawe waliushutumu upande wa Jamhuri kwa kuwasumbua na kuwa vigeugeu kwani wao ndiyo walioomba kesi hiyo itolewe Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kupelekwa mahakamani hapo kwa ajili ya kujadili umri.
Jaji Fauz aliipitia nakala ya barua iliyopelekwa Mahakama ya Rufaa na mawakili wa serikali na kutoa uamuzi kuwa kesi hiyo ipelekwe Mahakama ya Rufaa kwa ajili ya kutolewa upya uamuzi wa kujadili umri wa msanii huyo.

DK. CHENI AWATENGANISHA WAZAZI WAKE
Katika hali ya kushangaza, wazazi wa Lulu, hawakukaa pamoja, msanii wa filamu, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ ndiye aliyekaa katikati yao.
Jambo lililozidisha huzuni mahakamani hapo ni mdogo wake ambaye jina lake halikupatikana mara moja, kupelekwa kumsamilia sehemu aliyokuwa amekaa huku akiwa amezungukwa na maaskari magereza.
Hali hiyo ilimfanya Lulu amwage machozi kwa uchungu.
Kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Julai 09, mwaka huu kabla ya kuhamishiwa Mahakama ya Rufaa.

Thursday, June 28, 2012

Ni Italia na Uhispania katika fainali..Picha na matukio jana



 28 Juni, 2012 - Saa 21:13 GMT
Italia na Ujerumani
Ballotelli aliifungia Italia magoli mawili na kuifikisha nchi yake katika fainali ya Euro 2012
Mario Balotelli alifunga magoli mawili ya kupendeza mno na kuiwezesha timu yake ya Italia kuishangaza Ujerumani kwa kuifunga magoli 2-1 katika nusu fainali ya Euro 2012, na nafasi ya kucheza mechi ya fainali mjini Kiev dhidi ya Uhispania.
Mabao ya mshambulizi huyo wa klabu ya Manchester City ya England, aliingiza goli la kwanza wavuni kupitia kichwa, na pili kwa mkwaju wa kasi mno katika uwanja wa mjini Warsaw, na Italia kuwathibitishia Wajerumani katika kipindi cha kwanza kwamba ilikuwa na nia kamili ya kufika fainali.
Wajerumani, kufuatia mshituko, walianza kucheza kwa makini zaidi, lakini bao lao la penalti, ambalo lilipatikana katika dakika ya 92, kupitia Mesut Ozil, lilichelewa mno, na halikuweza kuwaokoa.
Italia kamwe hawajawahi kushindwa na Ujerumani katika mashindano makubwa, na wamefanikiwa sasa kucheza mechi nane dhidi ya Ujerumani pasipo kushindwa.
Hii sasa itakuwa mara ya tatu kwa Italia kuingia fainali za michuano hii ya mataifa ya Ulaya, na wataingia fainali kama timu inayodhaniwa kuwa dhaifu ikilinganishwa na mabingwa watetezi Uhispania.
Timu hii ya meneja Cesare Prandelli ilistahili ushindi, kwani sio tu waliweza kupambana na Ujerumani ambayo iliwashinda wapinzani wao kwa urahisi, bali pia walifunga mabao yao mapema katika kipindi cha kwanza.
Timu hiyo ya Azzurri ilikuwa na nafasi ya kujiongezea magoli, lakini ilicheza kwa tahadhari kwa kuhofia kwamba iwapo ingeliongoza mashambulizi zaidi dhidi ya Italia, kulikuwa na uwezekano wa ngome yao kuachwa ikiwa dhaifu, na Wajerumani kuwashambulia.

DIAMOND, WEMA WALIVYONASWA HOTELINI



Wema.
Diamond.
Hoteli ya Giraffe walimolala Diamond na Wema.
Gari la Wema likiwa eneo la hoteli ya Giraffe.

Gari la Diamond likiwa nje ya hoteli hiyo.
Musa Mateja na Imelda Mtema
NDIVYO ilivyokuwa, staa mkali wa filamu Bongo, Wema Sepetu na mwanamuziki wa Bongo Fleva ambaye kwa sasa yupo juu, Nasibu Abdul a.k.a Diamond ‘Plantinum’ wamenaswa katika hoteli yenye hadhi ya nyota tano Giraffe iliyopo Mbezi, jijini Dar es Salaam.
MESEJI YA KWANZA KWENYE SIMU YA PAPARAZI
Asubuhi ya Juni 26, 2012, ujumbe mfupi wa maneno (sms) uliingia kwenye simu ya paparazi wetu ukidondosha madai mazito kuwa, mastaa hao waliowahi kuwa wachumba na baadaye kumwagana kinomanoma, wako kwenye hoteli hiyo ‘wakiponda raha kwani kufa kwaja’.
Meseji hiyo ikafafanua: “Tena wapo toka jana, Wema yeye yupo toka alipomaliza ile shughuli yake na Omotola yule mdada wa Naijeria (Nigeria).”
MAPAPARAZI WAINGIA MZIGONI
Baada ya kupata ujumbe huo, waandishi wetu walikaa kama kamati mbele ya mhariri wao, wakaandaa zana mbalimbali zikiwemo kamera na vifaa vya kurekodia kwa ajili ya kufuatilia ukweli wa meseji hiyo.
GARI LA DIAMOND NJE YA HOTELI
Waandishi wetu walifika hotelini hapo saa 3:46 ambapo nje ya hoteli hiyo, mapaparazi hao walianza kuamini Platinum yupo ndani baada ya kuliona gari lake aina ya Toyota Prado, lakini katika kuzungusha makengeza yao hawakuweza kulitia machoni gari la Wema.
MBELE YA MAPOKEZI YA HOTELI
Mbele ya kaunta ya mapokezi, waandishi waliomba kuonana na Wema Sepetu.
Mtu wa Mapokezi: Nimwambie nani?
Musa: Mwambie baby wake.
Mtu wa Mapokezi: Baby wake yupi?
Musa: Musa Mateja.
Mtu wa Mapokezi alimtwangia simu Wema ambapo alipoambiwa ni Musa Mateja aliamuru asubiri eneo hilo mpaka atakapoitwa kwenda chumbani.
DIAMOND HUYO!
Waandishi wakiwa wamepiga kambi wakisubiri kuitwa, ghafla Diamond alishuka akiwa mbiombio kuelekea kwenye gari lake kama mtu anayewahi. Mapaparazi wetu walimfuata hadi kwenye gari ambapo alikuwa ameshaingia.
MSIKIE ALICHOSEMA
Bila kupoteza muda alisomewa mashitaka yake ‘eituzedi’ ambapo alivuta pumzi kwa nguvu kisha akafunguka:
“Mimi hata sijui kama Wema yupo hapa hotelini, kwani yupo hapa? Chumba namba ngapi? Mimi nilikuja kwenye mambo yangu, kwa sasa natunga mashairi ya wimbo mwingine kwa hiyo nilikuja tangu jana ili kufanya kazi yangu kwa ufanisi, unajua napenda kuwa sehemu yenye utulivu mkubwa.
“Unajua nini, nilikuwa Morogoro, nimerudi jana, nikaja hapa kumfuata Jeff, si unajua yule mshikaji wangu sana? Kuna wakati pia huwa nakuja pale kwenye hoteli moja ipo jirani na ofisini zenu, pale napo pazuri sana, nimewahi kulala. Ha! Ha! Ha! Musa bwana!”
MENEJA WA WEMA
Meneja wa Wema, Martin Kadinda naye alikutana na waandishi wetu ambapo alishtuka kumwona Diamond kwenye gari lake.
Martin: Khaa! Diamond unaweza kuja hapa hotelini halafu unaondoka usinitafute wakati unajua mimi nipo na tuna ishu yetu?
Diamond: (kicheko tu).
WAANDISHI WARUDI MAPOKEZI, WAITWA KWA WEMA
Baada ya kumalizana na Diamond waandishi wetu walirudi mapokezi ambapo walipelekwa kwenye chumba alichomo supastaa mwenye chemchemi za skendo Bongo, Wema na kumkuta akiwa na rafiki yake kipenzi (lakini asiyekubalika na mama yake), Snura Mushi.
Wema, baada ya kusomewa mashitaka yake alishtuka sana na kuonesha mshangao kusikia Diamond alilala hotelini hapo.
Alisema kuwa yeye ndiyo kwanza yuko kitandani na alikuwa amelala na Snura, habari ya Diamond kuwepo hotelini hapo anasikia kutoka kwa mapaparazi lakini yeye hajui chochote.
“Jamani mnavyoniona mimi hapa ndiyo kwanza nimeamka, hata nje sijatoka na watu wa kwanza kuongea nao ni nyinyi, mimi sijui kabisa kama huyo mtu yuko hapa. Kwanza alifuata nini hapa jamani?”
Amani: Sisi tulivyosikia alikuwa na wewe, sasa wewe tena unatuuliza sisi, tutajua vipi? Si ndiyo maana tumekuja?
Wema: Jamani kusema kweli… (akachukua simu na kumpigia mwanaume aliyedai ni mpenzi wake) dady, wamekuja waandishi hapa wanasema wamesikia nimelala na Diamond, we si tumeongea hadi usiku sana?
MASWALI MAGUMU
Inawezekana Diamond akafika hotelini hapo bila Wema kuwa na taarifa?
Ni kweli kwamba, Wema aliweka kambi pale kwa lengo la kujipumzisha tu akiwa na shoga yake Snura?
Utulivu anaodai Diamond aliufuata pale hotelini ulikosekana sehemu nyingine yoyote (hasa nyumbani) ikiwemo ufukweni?
Kwa nini Wema aliharakisha kumpigia simu huyo aliyemuita mpenzi wake kumwambia kuhusu waandishi kufuatilia habari ya kulala na Diamond wakati akidai walizungumza hadi usiku sana?
UKWELI UPO KWA WEMA, DIAMOND
Kwa maelezo yao hayo, bado ukweli unabaki kuwa siri yao. Hata hivyo, penzi halina siri, kama wanaficha, mapaparazi wapo macho kuwafuatilia na kama ni kweli wanatoka, siku moja mambo yatakuwa hadharani.

MAISHA YA UWOYA AIBU TUPU.



Irene Uwoya.

Uwoya akicheza na Steve Nyerere.

....Akiwa na mwanaume.
Shakoor Jongo na Imelda Mtema
MAISHA ya mwigizaji staa wa sinema za Bongo, Irene Uwoya bila kuwa na mumewe, Hamad Ndikumana 'Katauti' yanaonekana kuwa ya aibu tupu kufuatia siku za karibuni kubadilika tabia, hasa kwenye eneo la kujiheshimu, Amani linashuka sasa.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili siku za karibuni umegundua kuwa mambo mengi ya aibu ambayo staa huyo anayafanya, yanasababishwa na kutengana na mumewe ambaye kwa sasa amerudi kwao, Rwanda.
“Yaani Uwoya sasa hivi hana tofauti na msichana ambaye hafikirii kuolewa, amechangamka kila idara, hajali cha ndoa wala mume, anaonekana anajipongeza kwa ndoa yake kuvunjika,” alisema rafiki wa karibu wa Uwoya.
Tabia nyingine ambayo imegundulika kuwa staa huyo anayo kwa sasa ni kujiachia na waume za watu pamoja na waigizaji wenzake wa kiume huku ikidaiwa hachagui mahala popote yeye ni ‘kambi’.
“Siku hizi Uwoya anaweza kukaa sehemu, akamuegemea mwanaume ambaye ni mume wa mtu au akamfanyia msanii mwenzake vitendo ambavyo kwa mtu kama yeye aliye kwenye ndoa hatakiwi kuvifanya (angalia picha ukurasa wa mbele), hata kama ndoa yenyewe ilivunjika,” aliendelea kuanika rafiki huyo.
Akaendelea: Lakini bwana hata hao wanaume wenyewe wangekuwa wanaangalia; ya nini kuchezeana na msanii ambaye siku ikifika, mkatoka magazetini mnapiga kelele kulalamika?”
Rafiki huyo akaongeza: “Mabadiliko mengine ambayo Uwoya anaonekana kuwa nayo ni mavazi ambapo inadaiwa licha ya kuzoeleka kwa kuvaa mavazi ya nusu utupu akiwa na mumewe lakini kwa sasa amezidisha, anaweza kuvaa kigauni kifupi hadi akikaa nguo ya ndani inaonekana (picha ya aina hiyo iliwahi kutoka kwenye gazeti dada na hili, Ijumaa).
Mbali na mavazi, kujiachia na wanaume hadharani, imebainika kuwa, kwa sasa mwigizaji huyo ndiye anayeongozwa kwa kutetwa na marafiki zake wa karibu, wengi wakionesha kutomuunga mkono kufuatia kitendo chake cha kukubali ndoa yake ivunjike.
Hilo lilionekana hivi karibuni alipotinga kwenye Hotel Hyatt Kilimanjaro Kempinski, jijini Dar es Salaam ambapo staa mwenzake, Wema Sepetu alikuwa akizindua filamu ya Superstar.
Uwoya alitinga ukumbini akiwa amevaa vazi jeusi na la ajabu, chini alivaa soski nyeusi tu bila viatu huku kucha za vidole vya mikononi zikiwa ndefu na kupakwa rangi nyekundu hivyo kuonekana kama mtu wa kwenye filama za kutisha (angalia picha ukurasa wa mbele).
“Hivi Irene amevaaje leo jamani? Ina maana kutoka moyoni ameona vile ni sawa?” alisikika akihoji mmoja wa mastaa wa kike Bongo.
Hata hivyo, Uwoya alipopigiwa simu juzi, Jumanne, hakupatikana.

Wednesday, June 27, 2012

USIKU WA WEMA HAIJATOKEA...PICHA NA MATUKIO











Stori: Shakoor Jongo na Musa Mateja
JUNI 23, mwaka huu ndani ya Hoteli ya Hyyat Kilimanjaro Kempinski iliyopo Posta jijini Dar, staa wa filamu, Wema Isaac Sepetu alizindua filamu yake ya Super Star na kufanya mambo makubwa ambapo wadau walisema haijawahi kutokea Bongo, Risasi Mchanganyiko lilishuhudia.
Usiku huo ambao Wema aliutumia kuzindua filamu hiyo uliwakutanisha mastaa kibao na watu wengine mashuhuri ambapo vituko vya hapa na pale vilitawala.
Hakukuwa na kiingilio katika uzinduzi huo lakini ilikuwa ni lazima mtu apewe kadi maalum au atumiwe ujumbe wa simu wa mualiko.
Kwa upande wa burudani, wasanii kutoka nyumba ya vipaji, THT, msanii wa filamu anayefanya muziki wa mduara, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ na mwanadada wa Bongo Fleva, Sarah Kaisi ‘Shaa’ walitumbuiza katika uzinduzi huo.
REDI KAPETI ILIKUWEPO
Kama kawa, zulia jekundu liliwekwa kwa ajili ya wageni waalikwa kupita na kupiga picha za mapozi tofauti.
KULA, KUNYWA BURE
Ndani ya ukumbi huo, vinywaji na vyakula vilikuwa bure kwa kila aliyetinga kushuhudia uzinduzi wa filamu hiyo inayodaiwa kuwa na matukio ya kweli yanayomhusu staa huyo aliyetwaa taji la urembo la Tanzania mwaka 2006.
VITUKO
Mastaa kama vile, Vincent Kigosi ‘Ray’ Halima Yahya ‘Davina’ na Jacob Steven ‘JB’ waliwaongoza wengine kukata nyonga zao ili kupamba usiku huo wa Wema.
Aidha, mwanamitindo Jacqueline Patrick, Belina Mgeni na mastaa wengine waliokuwa wamevalia viatu virefu walishindwa kujiachia navyo hivyo kulazimika kuvivua ili wawe huru kucheza muziki wa Kwaito.
Katika kuweka vionjo, mastaa hao walishindana kucheza huku wengine wakichuana katika kutunza ambapo Ray na Steven Mangere ‘Steve Nyerere’ walichukua nafasi ya upedeshee.
UZINDUZI RASMI WA FILAMU
Huku watu wakiendelea kula bata, mshereheshaji wa hafla hiyo ambaye ni Mtangazaji wa Redio Times ya jijini Dar, Khadija Shaibu ‘Dida’ aliwaomba wageni waalikwa kuingia katika ukumbi mwingine kwa ajili ya kuzindua filamu hiyo.
“Wageni waalikwa nawaomba muingie katika ukumbini wa Level Eight kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa filamu yetu,” alisikika Dida akisema.
MINONG’ONO KUHUSU OMOTOLA YATAWALA
Wakati muda ‘ukitaradadi’, minong’ono ilianza kutanda ukumbini hapo kwamba Wema kawapiga wadau ‘changa la macho’ juu ya ujio wa staa kutoka Nigeria, Omotola Jalade.
“Unafanya mchezo nini kumleta staa kutoka Nigeria, aliweza marehemu Kanumba tu tena kwa kusaidiwa na Steps siyo Wema,” alisikika akibwatuka staa mmoja wa tasnia ya filamu Bongo.
OMOTOLA ATUA USIKU WA MANANE
Wakati kila aliyekuwa katika sherehe hiyo akiamini Omotola asingeweza kufika Bongo, mishale ya saa 9:00 usiku MC alitangaza kuwa muda wa kwenda kumpokea mgeni huyo umewadia hivyo msafara wa kwenda Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere ulianza.
Ilipotimu saa 9: 15 usiku, Omotola alitua na kumfanya Wema ‘kupiga bao’ kwa kudhihirisha kwamba hakuwa akitania aliposema anamleta staa huyo.
Hata hivyo, Omotola alipotinga ukumbini alikuta baadhi ya wadau wa filamu walishaondoka kwa kuwa muda ulikuwa umekwenda sana.
KALI ZAIDI
Mbali na kukodi ukumbi wa hoteli hiyo, Wema pia alikuwa amemkodia Omotola vyumba viwili, kimoja kwa ajili ya kulala na kingine kwa ajili ya kubadilishia nguo na kupambwa (kufanyiwa make-up).
Hali kadhalika, Wema naye alikuwa na vyumba viwili katika hoteli hiyo vilivyokuwa na matumizi kama ya Omotola.
GIRAFFE HOTELI
Kama vile haitoshi, uzinduzi wa filamu hiyo uliendelea usiku wa siku ya pili Juni 23, mwaka huu katika Hoteli ya Giraffe iliyopo Mbezi Beach jijini Dar ambapo Omotola alikuwa mgeni rasmi.
Huko nako Wema na Omotola walimiliki vyumba viwiliviwili kwa ajili ya kujipamba na kulala.
Katika ukumbi wa hoteli hiyo, Bendi ya Sky Night ilitumbuiza na Mtangazaji Benny Kinyaiya alikuwa MC ambapo watu wa kawaida walitakiwa kulipa shilingi 30,000 kushuhudia uzinduzi huo.
Kabla ya uzinduzi, mabibi wanaoshiriki Shindano la Bibi Bomba linaloendeshwa na Kituo cha Clouds TV walipita katika redi kapeti na kuonesha manjonjo yao.
Baada ya hapo, MC alimkaribisha Wema ambaye alisema machache kisha akamkaribisha mgeni wake kunena chochote kabla ya kuzindua rasmi filamu hiyo na kuwaacha watu wakiiangalia.
Baada ya tukio hilo, wadau wengine wakiwemo mastaa wa Bongo walionesha vituko vingine kwa kugombania kupiga picha na Omotola ambapo kutokana na vurugu, watu walitakiwa kupanga mstari ili kutimiza zoezi hilo.
Wakati shughuli hiyo ilipofikia kikomo, Wema na baadhi ya watu mashuhuri walienda katika ufukwe wa Ngalawa uliopo karibu na hoteli hiyo ambako waliendelea kujiachia.
Kwa tukio hili, Wema amevunja rekodi ya kutengeneza filamu kwa gharama kubwa lakini pia amevunja rekodi kwa kufanya pati ya nguvu.
MASWALI MAGUMU
Pamoja na Wema kufanikisha uzinduzi huo, wadau wamekuwa wakijiuliza staa huyo amepata wapi fedha za kufanyia mambo yote hayo.
WEMA ANASEMAJE?
Risasi Mchanganyiko, lilimuuliza Wema gharama alizotumia kukodi ukumbi huo ambapo hakuwa tayari kuweka bayana zaidi ya kutaja gharama za maandalizi ya filamu hiyo ambayo ni shilingi milioni 68.

Wahamiaji 42 wafa kwenye lori Tanzania

 27 Juni, 2012 - Saa 15:21 GMT

Tanzania
Tanzania
Wahamiaji haramu arobaini na wawili wamepatikana wakiwa wamekufa ndani ya lori walimokuwa wakisafiria katika mkoa wa Dodoma, nchini Tanzania.
Naibu waziri wa mambo ya ndani wa Tanzania, Pereira Silima, amesema kuwa watu hao waliokuwa wamesongamana ndani ya lori waliaga dunia kutokana ukosefu wa hewa safi.
''Taarifa tuliyopata ni kwamba kulikuwa na wasafiri waliokuwa wakisafirishwa kwenye lori, ambalo lilikuwa kama kontena na halikuwa na hewa ya kutosha''.Bwana Silima ameambia BBC.

wahamiaji walikuwa wanatoka Ethiopia

Amesema wahamiaji hao haramu kutoka Ethiopia walikuwa wakijaribu kuingia Malawi.
Kulingana na bwana Silima wahamiaji hao walianza kufariki dunia wakiwa safarini. Jihudi za wahamiaji hao kumjulisha dereva kuhusiana na hali yao hazikufanikiwa, na hivyo kusababisha maafa ya watu arobaini na moja ndani ya lori hilo.
Kulingana na naibu waziri huyo wa mambo ya ndani tukio hilo lilifanyika Jumatatu usiku. Na baada ya dereva huyo kugundua kuwa watu wamefariki, aliondoa miili yao na kuitupa nje kabla ya kutoweka.
Mtu mmoja alifariki dunia akifanyiwa matibabu katika hospitali ya mkoa mjini Dodoma.

uhamiaji haramu umeenea

Polisi nchini Tanzania wamesema wanamsaka dereva huyo ambaye alitoroka punde tu baada ya kushusha miili ya wahamiaji hao haramu.
Biashara ya kuwasafirisha wahamiaji haramu hasa wanaotoka nchi za Somalia na Ethiopia kupitia Tanzania imeenea sana. Wengi huelekea mataifa ya kusini mwa Africa kutafuta maisha bora.

Dr. ULIMBOKA ATEKWA NA KUUMIZWA VIBAYA.PICHA NA MATUKIO...

Wednesday, June 27, 2012

Dr. Ulimbika kabla ya tukio


hali ya Dr. Ulimboka hali aliyokutwa nayo

Akipakizwa kwenye gari

Nesi akilisukuma ambulance

wauguzi na madaktari wakijadiliana jambo

Kiongozi wa madakitari nchini, Dk. Stephen Ulimboka, leo ameokotwa maeneo ya Mabwe Pande, Dar es Salaam, akiwa hoi baada ya kupigwa na watu wasiofahamika.
Kitendo hicho kilisababisha kusimama kabisa kwa huduma katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya madaktari, wauguzi na wahudumu wengine kukasirishwa na kitendo hicho.
Madaktari wameishtumu serikali na jeshi la polisi kwa kile walichokiita kushiriki katika jaribio la kumwua kiongozi wao.

jeshi la polisi launda jopo maalum kwa upelelezi wa tukio la utekaji nyara wa Dr. Ulimboka

Saturday, June 23, 2012

MAMA KANUMBA ANUNUA...

 Imelda Mtema na Erick Evarist
ZIMEKATIKA siku 75 tangu kufariki dunia kwa supastaa wa filamu za Bongo, Steven Charles Kanumba, Aprili 7, 2012. Mama mzazi wa marehemu huyo, Flora Mtegoa mambo yamemnyookea ambapo amenunua jumba kubwa la kifahari, Risasi Jumamosi linakuwa la kwanza kuripoti.
CHANZO CHATEMA NYETI
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, mjengo huo upo Kimara Temboni jijini Dar es Salaam ambapo mama huyo na familia yake (akiwemo Seth Bosco) wamehamia.
Sanjari na wao, pia magari matatu ya marehemu, Toyota Hiace, Toyota Lexus na Toyota GX 110 yamepiga kambi huko, kila moja likiwa na sehemu yake ya kuegesha.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, kwa sasa mama Kanumba hana makazi tena pale Sinza Kijiweni ambako ndiko palipofanyikia msiba wa mwanaye hadi kuhitimisha na arobaini yake.
KUNA USIRI
Chanzo kikadai kuwa kuhama kwa mama huyo na familia yake kutoka Sinza kwenda Temboni kumegubikwa na usiri bila kufafanua siri hiyo inatokana na nini!
MAPAPARAZI WAINGIA MZIGONI KUCHUNGUZA
Baada ya gazeti hili kuzidaka nyeti hizo, Alhamisi ya Juni 21, 2012 lilituma timu ya waandishi wake kwenda kupata uhakika wa madai hayo na kujiridhisha kabla ya gazeti halijakwenda mitamboni.
NJE YA NYUMBA
Ndani ya geti kuu la nyumba hiyo yenye bati la kijani, alikutwa mdogo wa marehemu Kanumba, Seth Bosco akipata chai huku upepo mwanana ukimpuliza. Mama Kanumba alikuwa akiendelea na shughuli zake za kawaida.
Mbali na kuwaona wawili hao, mapaparazi wetu waliendelea na uchunguzi wao ambapo waliipiga raundi nyumba hiyo na kujionea magari yote matatu ya marehemu  yakiwa yamepaki huku jamaa mmoja akiwa juu ya bati kuweka dishi la televisheni la ‘kuangalizia’ Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya ‘Euro’ yanayoendelea kwa sasa nchini Poland na Ukraine.
Makachero wetu walipojiridhisha kuwa mama Kanumba ndiyo kaweka makazi yake mapya, lilipiga picha za kumwaga kisha lilimwendea hewani Seth na kuzungumza naye ili kupata ukweli mwingine.
SAUTI YA SETH KUTOKEA TEMBONI
Paparazi: Mambo Seth?
Seth: Poa tu, nani mwenzangu?
Paparazi: Unaongea na Risasi Jumamosi hapa.
Seth: Enhe, lete habari.
Paparazi: Inasemekana mmehama pale Vatican, mmehamia wapi?
Seth: Aaa, tumehamia Temboni huku.
Paparazi: Ni kweli huko mmenunua nyumba?
Seth: Ni kweli.
Paparazi: Shilingi ngapi?
Seth: Mh! Hilo swali anayeweza kujibu ni mama kwamba ni shilingi ngapi na mambo mengine yote.
Risasi Jumamosi lilipomsaka mama Kanumba kwa kutumia simu yake ya mkononi, hakupatikana hewani siku hiyo.
MJENGO WA BEI MBAYA
Hata hivyo, Risasi Jumamosi lilifanya uchunguzi na kunyaka baadhi ya nyaraka zinazoonesha kuwa mjengo huo umenunuliwa kwa shilingi milioni themanini (80,000,000) za Kibongo.
MASTAA HAWAJUI
Gazeti hili lilijaribu kufanya mawasiliano na baadhi ya mastaa wa filamu Bongo kama wanajua mama yao huyo amehama Sinza lakini kila aliyeulizwa hakuwa anafahamu na kuwa ‘sapraizi’ kwake.
Mwanyekiti wa Klabu ya Bongo Movie, Jacob Steve ‘JB’ alipovutiwa uzi na kuulizwa alisema hajui kama mama Kanumba amehama Sinza.
HII HAPA SAUTI YAKE
“Amehama pale? Duu! Mimi sijui kaka.”
MWAKIFAMBA AKIWA NJIANI KWENDA SINZA
Naye Mwenyekiti wa Shirikisho la Filamu Bongo, Simon Mwakifamba alipopigiwa simu kuulizwa, akajibu anaamini mama huyo bado yupo Sinza, na yeye mwenyewe alipanga kwenda siku hiyo ya Alhamisi jioni ili akamjulie hali.

Thursday, June 21, 2012

Ali kiba afungukia skendo ya kulawitiwa

Ali Kiba.
Erick Evarist
WAKATI stori za kulawitiwa kwa staa wa Bongo Fleva, Ali Kiba zikitokota chini kwa chini, mwenyewe ameibuka na kukanusha kuwa si za kweli.
Akizungumza na mtandao mmoja Bongo, Ali Kiba amekanusha madai hayo na kufafanua kuwa, uvumi huo ulichagizwa na rafiki yake mmoja wa karibu ambaye walikuwa wakiishi naye.
“Si kweli bwana, hizo stori si za kweli, jamaa tulimtimua home baada ya kugundua ana tabia ya udokozi ndipo akaamua kupakaza stori kama hizo,” alisema Ali Kiba

JACK DUSTAN AWEKWA KINYUMBA HOTELINI


 Jacqueline Dustan ‘Jack wa Maisha Plus’.
Na Gladness Mallya
MSHIRIKI wa Shindano la Maisha Plus Season II, Jacqueline Dustan ‘Jack wa Maisha Plus’ anadaiwa kuwekwa kinyumba hotelini kwa muda wa wiki moja.
Kikizungumza chanzo makini ambacho ni rafiki wa karibu na Jack kilisema kuwa mwanadada huyo aliwekwa katika Hoteli ya Danfrense iliyopo maeneo ya Sinza White Inn, Dar ambapo alikaa na mwanaume mmoja ambaye hakujulikana jina anayeishi nchini Denmark.
“Yaani Jack alikaa hotelini kwa muda wa wiki moja kwa ajili ya huyo mwanaume wake, naona huyo ndiyo anampa mkwanja ‘so’ yupo tayari kwa lolote,” kilisema chanzo.
Jack alipopatikana alifunguka: “Ni kweli nimekaa hotelini na mwanaume wangu anayeishi Denmark, siwezi kumtaja, alikuja kwa ajili yangu. Pia siwezi kusema ni mchumba wangu kwa sababu bado hajajitambulisha kwetu lakini naweza kusema ni mpenzi wangu tu na ameshaondoka.”

50 CENT NAE ATOA MAONI YAKE JUU YA BEEF YA BRIZZY NA DRIZZY.



G. Unit C.E.O 50 Cent analinganisha beef ya Drake na Chris Brown iko kiraha sana na pia inawapaisha, akiongelea mzozo huo wakati akipiga story na LA Leakers, 50 cent hakujua chochote kuhusu hilo aliona picha ndipo aliposhangaa sana kusikia washikaji wamerushiana chupa katika club ya usiku huko New York. “Hivi ni kweli ule ugomvi umesababishwa na msichana? (Rihanna), Hapana sidhani basi wanakitu chao katika music wanajuana wenyewe” Alisema Fif. Ni mbaya sana sikudhani kama wanaweza kuhusishwa katika aina hiyo ya ugomvi, Meek Mill, Chriss Brown alafu Drake, sikuwahi kufikiria kati yao kuna mpiganaji, lakini ukiangalia itakuwa ni kimuziki sana sana” Aliendelea kufunguka Fid a.k.a Fif.

Wawili waachiliwa na maharamia Somalia


 21 Juni, 2012 - Saa 14:01 GMT

Calitz na mumewe Bwana Pelizzari baada ya kuachiliwa huru na maharamia
Raia wawili wa Afrika Kusini ambao wamekuwa wakishikiliwa mateka na Maharamia wa Kisomali wameachiliwa huru.
Wawili hao, Bi Calitz na Bwana Pelizzari, ambao ni mtu na mkewe wamekuwa wakizuiliwa nchini Somalia kwa miezi 20.
Waziri wa ulinzi wa Somalia amesema jeshi na walinda usalama walikuwa wameanza harakati za kuwaokoa watu hao siku ya Jumatano usiku.
Bi Calitz na Bwana Pelizzari walitekwa nyara mwezi Oktoba mwaka 2010 walipokuwa ndani ya chombo chao katika bahari hindi.
Hata hivyo Waziri wa ulinzi wa Somalia Hussein Arab Isse hakufichua kama kikombozi chochote kililipwa kabla ya wawili hao kuachiliwa.
Awali maharamia hao walikuwa wametaka kulipwa dola milioni 10 kabla ya kuwaachilia raia hao wawili wa Afrika Kusini.
Mtu huyo na mkewe walijitokeza wakiwa na waziri huyo katika mkutano wa waandishi habari.
Walisema walikuwa na furaha na walikuwa wanatarajia kujiunga na familia yao.
Umoja wa ulaya unasema kwa wakati huu kuna jumpla ya mateka 213 ambao bado wanazuiliwa na maharamia.

LATEST ON BIG BROTHER STARGAME

 (Day 45)

Wati.
Goldie.
Keagan.
Prezzo and Goldie.
Talia.
-----
LATEST ON BIG BROTHER STARGAME (Day 45)
After a traumatic four weeks marred by drama and violence, Big Brother organised a Therapist for the traumatised Upvillers. The Housemates spoke at length with the Therapist, during a private session conducted in the Upville lounge. In the last fourteen days, four Housemates have been disqualified from StarGame after their verbal arguments turned physical.
There has also been a lot of confusion in Upville since Maneta and Roki were disqualified regarding the Evictions on Sunday night as many of the Housemates were not sure whether Evictions would continue as planned or not. Big Brother then put the Housemates out of their misery and notified them that despite Maneta and Rookie’s disqualification, Evictions will go on as planned this Sunday.
Meanwhile, after saving Prezzo from the Eviction gallows, Goldie feels she may have made a mistake. On Monday, Prezzo, Maneta and Barbz made up the Nominations list, however, Goldie exercised her Head of House powers to save her boyfriend Prezzo and put Keitta on the chopping block instead. Goldie however broke down during one of her Diary Room sessions and revealed how gutted she is that she betrayed her friend, Barbz!
In the Downville Diary Room, things got heated when a fight broke out between sisters, Talia and Tamara. Tamara complained that she hasn't had any one on one time with her sister in a while.  Talia replied by saying that she is tired of living in her sister’s shadow and that she wants to be an individual and be able to interact freely with other Housemates.
Housemates were also busy with preparations for their task presentation on Thursday evening for which they wagered 100%. Big Brother commissioned housemates to pick a partner and pamper each other with beauty treatments including manicures, pedicures and facials.

Set to get the party started in the Big Brother House this weekend is the energetic, fun and super cool DJ Malick. The talented Malawian is the host of Gowelo Beats and Crush Grooves on Power 101. He will also be keeping the audience on their feet at the live Sunday Eviction Show while Ghanaian rapper and songwriter M.anifest will be performing on the night.
The 91 day reality super-series Big Brother StarGame, produced for M-Net’s AfricaMagic, is being screened live 24/7 on DStv channels 197 & 198. For more information on the show, you can log on to   www.africamagic.tv/bigbrother