Sunday, August 19, 2012

SALAMU ZA EID MUBARAK KUTOKA KWA MHE LOWASSA KWA WAISLAMU NA WATANZANIA WOTE

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa.
LEO ni sikukuu ya Eid Elfitr, ambapo ndugu zetu Waislamu wameungana na Waislamu duniani kote kuishrehekea sikukuu hii tukufu iliyoanza baada ya kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Binafsi kwa niaba ya familia yangu na wananchi wote wa Jimbo la Monduli, Napenda kuchukua fursa hii kuwatakia Watanzania wote mkono wa Eid Elfitr.
Kwa wagonjwa na wenye shida mbalimbali nachukua pia fursa hii kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu awape tahafifu ili kwa pamoja tusherehekee sikukuu hii tukufu kwa wenzetu Waislamu. 
Na pia Nawaombea mpate afuene ili kwa pamoja tuendelee na jukumu la pamoja la kuijenga nchi yetu pamoja na kumsaidia Mh Rais Jakaya Kikwete katika kuitekeleza vyema ilani ya Chama Chama Mapinduzi, ambayo inahimiza kuilinda amani ya nchi yetu kama tunu pekee tuliyorithi toka kwa waasisi wetu wa taifa Baba wa Taifa Mwalimu Julius K .Nyerere na Mzee wetu Sheikh Abeid Aman Karume. 
Ambapo leo hii dunia inajua na Tanzania inajua Amani tuliyonayo inatokana na misingi imara tuliyojengewa kama taifa na kufanikiwa kuheshimiana na kuvumiliana licha ya tofauti zetu za kikabila, kidini na kiimani, lakini wote tunaabudu bila kuvunja amani yetu na sheria za nchi.
Kwa pamoja naomba niwatakie siku njema na Asanteni sana Wanatanzia wenzangu

EID MUBARAK WOTE NAWAPENDA SANA...

No comments:

Post a Comment