Friday, July 6, 2012

RAY aichomolea ndoa


Vincent Kigosi ‘Ray’.

STAA wa sinema za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ ameweka wazi kuwa watu wanaomsumbua juu ya suala la kuoa, watasubiri sana kwani hana mpango huo.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Ray alifunguka kuwa staili ya maisha yake ndiyo inayomfanya aishi anavyotaka hivyo suala la kuoa halipo kwenye akili yake.
Alisema amekuwa akishauriwa na ndugu, jamaa na marafiki afanye hivyo ili yasije yakamkuta kama yaliyomkuta swahiba wake marehemu Steven Kanumba aliyefariki dunia akiwa hajaoa wala hana mtoto lakini yeye hana mzuka na mambo hayo.
“Sina mpango wa kuoa bwana, wanaotaka kuoa waoe tu na mimi nitachangia michango lakini mimi sipo tayari kwa sasa,” alisema Ray ambaye sasa ana umri wa miaka 32.

No comments:

Post a Comment