Friday, July 20, 2012

TATUU ZA QUEEN SUZY WA NGWASUMA ZAPAGAWISHA MASHABIKI MORO

Baadhi ya tatuu za Queen Suzy.
...Akionyesha machejo jukwaani.
Mwandishi wa mtandao huu akimhoji Suzy (katikati).  Kulia ni mnenguaji mwenzake.
...Akionyesha matindo ya aina yake kwa kupiga msamba.
...Akijtayarisha  kuonyesha tatuu zake za nyuma.
MNENGUAJI nyota wa bendi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma',  Suzan Godwin Chubwa  'Queen Suzy' hivi karibuni alipagawisha mashabiki katika Manispaa ya Morogoro wakati wa hafla ya kumtafuta Miss Morogoro kutokana na tatuu zake maridadi alizojichora mwilini.
Hafla hiyo ilifanyika Morogoro Hotel.
Akizungumza na mtandao huu, mrembo huyo ambaye kabla ya kujiunga na bendi hiyo alikuwa na bendi ya African Stars wajulikanao kama ‘Twanga Pepeta’, alisema mapambo hayo ni kwa ajili ya kuwachengua mashabiki  wake wakati akinengua jukwaani.

No comments:

Post a Comment