Sunday, September 23, 2012

Afande aacha kazi ya ulinzi uwanjani na kugeuka paparazi‏mmCheki alichokifanya

Afande akipiga picha kwa kutumia simu yake
Hapa akimpiga picha aliyekuwa kocha wa yanga Tom Saintfiet kabla ya kutimuliawa
Askari mmoja ambaye anasadikiwa kuwa ni shabiki mkubwa wa timu ya Yanga, Jumatano iliyopita alilazimika kuacha kazi ya ulinzi na kusukumana na mapaparazi akiwapiga picha wachezaji na kocha wa Yanga kwa kutumia kamera ya simu yake.
Baadhi ya maaskari wa Tanzania ni mashabiki wakubwa wa timu za Simba na Yanga na kujikuta wakionyesha mapenzi yao bila kujali kama wako kazini, katika mchezo huo wa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom kati ya wenyeji Mtibwa Sugar na Yanga uliopigwa Jumatano iliyopita ndani ya Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogororo, Yanga ilichapwa bao 3-0, ambapo miongoni wa watu walioonekna kusononeka na kichapo hicho ni Afande huyo wa kikosi cha kutuliza ghasia.
Mashabiki wa Simba waliopata kumshuhudia kijana huyo wa I.G.P Said Mwema walimzomea na kumtupia maneno ya kejeli hali iliyomfanya kusitisha zoezi hilo na kuweka simu yake mfukoni na kuchukua kilungua chake na kuendelea na kazi.                 
PICHA HABARI NA DUNSTAN SHEKIDELE, GPL MOROGORO

No comments:

Post a Comment