Thursday, September 27, 2012

CHUZ ADAIWA KUMSUSA MSANII WAKE MGONJWA

Stori: Na Gladness Mallya
MSANII mkongwe Bongo, Juma Ally Salim ‘Mzee Kankaa’ amemrushia lawama Mkurugenzi wa Tuesday Entertainment, Tuesday Kihangala ‘Chuz’ kwamba amemsusa baada ya kushikwa na ugonjwa wa kupooza.
Akizungumza kwa kuchanganya maneno kutokana na tatizo hilo, Mzee Kankaa alisema usiku wa Aprili 7, mwaka huu ndipo alipokumbwa na ugonjwa huo ambapo alipooza upande mmoja na kupoteza kumbukumbu.
“Baada ya kupatwa ugonjwa huu, Chuz ambaye nilifanya naye kazi kwa usahihi kwenye Tamthiliya ya Jumba la Dhahabu ambayo kwa sasa ipo madukani, alifika kunijulia hali mara moja tu, tena kwa sekunde chache kisha akaondoka na hajawahi kurudi tena,” alisema kwa masikitiko mzee huyo.
Chuz alipopatikana kwa njia ya simu yake ya kiganjani, alikuwa na haya ya kusema: “Sijamsusa Mzee Kankaa, namheshimu sana tatizo mambo yalikuwa mengi ndiyo maana nikashindwa kwenda kumuona tena, lakini nitakwenda.”

No comments:

Post a Comment