Saturday, April 28, 2012

Afisa hataki Israil ishambulie Iran


Mkuu wa zamani wa Shirika la Ujasusi la Israil, Shin Bet, amemlaumu Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, pamoja na Waziri wa Ulinzi, Ehud Barak, kwamba hawawaambii ukweli wananchi wa Israil kuhusu Iran.
Yuval Diskin, mkuu wa zamani wa Shin Bet

Yuval Diskin, amewashutumu wanasiasa hao wawili, kuwa wanafanya uamuzi kwa msingi wa itikadi zao, na alisema hakuna ukweli kwenye hoja yao, kwamba endapo Israil itachukua hatua za kijeshi, Iran haitatengeneza bomu la nuklia.
Juma lilopita mkuu wa jeshi wa Israil aliliambia gazeti moja la nchi hiyo kwamba hafikiri kuwa Iran itatengeneza silaha za nuklia.
Mwezi uliopita, mkuu wa shirika jengine la ujasusi la Israil, Mossad, piya alisema hadharani kuwa anapinga shambulio dhidi ya Iran.

No comments:

Post a Comment