Saturday, April 28, 2012

BAADHI YA MARAIS WA (EAC) WAWASILI JIJINI ARUSHA

Mhe. Mwai Kibaki, Rais wa Kenya akipokelewa na Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) jana kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika mjini Arusha tarehe 28 Aprili, 2012.

Mhe. Rais Kibaki akifurahia burudani ya ngoma mara baada ya kuwasili KIA.

Mhe. Rais Kibaki akiwa na wenyeji wake Mhe. Membe (kulia) na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Samwel Sitta (kushoto) mara baada ya kuwasili KIA

Mhe. Yoweri Museveni, Rais wa Uganda akisalimiana na Mhe. Samwel Sitta, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki mara baada ya kuwasili KIA kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki tarehe 28 Aprili, 2012.

KITIVO CHA ELIMU UDOM CHAIBUKA NA USHINDI WA VIKAPU 58 KWA 53 DHIDI YA DODOMA SPURS KATIKA LIGI YA MPIRA WA KIKAPU MKOANI DODOMA

Mchezaji wa timu ya Kitivo cha elimu cha Chuo Kikuu Cha Dodoma akijaribu kufunga katika mechi ya ligi ya mpira wa kikapu iliyoanza leo na timu hiyo ya walimu kuibuka washindi kwa vikapu 58 kwa 53 dhidi ya Timu ya Kikapu Ya Mkoa Wa Dodoma

Mpira ukiingia kwenye nyavu na kupelekea timu ya kitivo cha elimu cha Chuo Kikuu Cha Dodoma kushinda

Mchezaji wa timu ya Kitivo cha Elimu Cha Chuo Kikuu Cha Dodoma akiokoa hatari goli kwake

Kashikashi ikiendelea hapo huku wengine wakitaka kushinda huku wengine wakitaka kuokoa goli lisiingie

Mchezaji wa Timu ya Mkoa alipoipatia timu goli katika ligi ya mpira wa kikapu iliyoanza leo katika viwanja vya kitivo cha sayansi ya Jamii, Sanaa na Lugha cha Chuo Kikuu Cha Dodoma

Mchezaji wa Timu ya Kikapu ya Dodoma Spurs (Timu ya Mkoa) akijaribu kumpita Mchezaji wa timu ya kikapu ya kitivo cha elimu cha chuo kikuu cha Dodoma katika mchezo wa ligi ya mpira wa kikapu iliyoanza leo na timu ya Kitivo cha Elimu cha Chuo Kikuu Cha Dodoma Chaibuka Mshindi Kwa Vikapu 58 kwa 53 Dhidi ya Timu ya Mkoa (DODOMA SPURS)

 Mpira ukielekea nyavuni hapo

Benchi la Makamisaa likifuatilia Mchezo huo Kwa Makini

 Baadhi ya Wanafunzi na Wadau wengine wakifuatilia mchezo huo uliokuwa ukichezwa kati ya Timu ya Mpira ya Kikapu kutoka Kitivo Cha Elimu Cha Chuo Kikuu Cha Dodoma Na Timu ya Dodoma Spurs (Timu ya Mkoa) ambapo timu ya kitivo cha elimu cha Chuo Kikuu Cha Dodoma iliibuka na ushindi wa Vikapu 58 kwa 53 dhidi ya Timu ya Mkoa Wa Dodoma (DODOMA SPURS) katika ligi ya mpira wa kikapu inayoendelea kufanyika katika viwanja vya Kitivo Cha Sayansi ya Jamii,Sanaa na Lugha cha Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM)

No comments:

Post a Comment