Sunday, April 29, 2012


Mlipuko waua watu 70 Hama Syria

 


Watu takriban 70 wameuawa katika shambulio kwenye nyumba moja katika eneo la Hama, hayo ni kwa mujibu wa wanahakarakati wa Syria.


Wanasema nyumba kadhaa katika wilaya ya Masha at-Tayyar kusini mwa Hama ziliharibiwa kutokana na shambulio kubwa.


Shirika la habari la serikali linasema kuwa watu 16 waliuawa ndani ya nyumba iliyokuwa ikitumiwa kama kiwanda cha kutengeneza mabomu na "kundi la magaidi".


Makabiliano hayo yametokea licha ya Umoja wa Mataifa kutaka mapigano yasitishwe - ikiwa ni mpango wa amani uliopendekezwa na mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Kiarabu Kofi Annan.

No comments:

Post a Comment