Monday, May 21, 2012

FLAVIANA MATATA ATOA MSAADA WA VIFAA VYA KUJIOKOLEA MAJINI

JANA 21
Historia imewekwa leo na Flaviana Matata alipokabidhi msaada wa maboya (life vests) 500 kwa Shirika la Meli la Taifa (Marine Services Co Ltd) kama sehemu ya kumbukumbu ya MV Bukoba - ambapo ni miaka 16 tangu Meli hiyo ilipozama na kuua watu takriban 1,000 akiwemo pamoja na mama yake Flaviana.
  Flaviana Matata akikabidhi msaada wa maboya 500 kwa mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Mwanza, Elias Makori kulia ikiwa ni kumbukumbu ya miaka 16 ya ajari ya meli ya MV Bukoba, anayeshuhudia ni Meneja Masoko na Biashara wa Shirika la usafirishaji wa majini mkoani Mwanza la Marine Service, Kapten Obadia Nkongoki. Igoma jijini Mwanza.
 Flaviana Matata akishindwa kujizuia na kuangua kilio wakati wa ibaada ya kumbukumbu ya miaka 16 ya ajari ya meli ya MV Bukoba alipotembelea baadhi ya makaburi ya watu waliopoteza maisha katika ajari hiyo yaliyopi Igoma jijini Mwanza, katika ajali hiyo Flaviana alimpoteza pia mama yake mzazi. 
 Flaviana akionesha moja ya maboya yenye nembo ya foundation yake aliyokabidhi katika kumbukumbu ya miaka 16 ya ajali ya MV Bukoba ikiwa ni kampeni yake ya kupunguza ajari za majini hapa nchini.
 Flaviana na wageni wakiweka  mashada kwenye makaburi ya waliofariki kwenye ajali hiyo Igoma Mwanza

Waombolezaji wengine waliofiwa na ndugu zao wakiombea marehemu wa ajali hiyo.
---
Mwanamitindo wa kimataifa Flaviana Matata ametoa msaada wa vifaa mbalimbali vya kuokolea maisha ya watu katika vyombo vya usafiri wa  majiambavyo vimelengwa maalum kwa Ziwa Viktoria mjini Mwanza. Msaada wa vifaa hivyo umeelekezwa katika shirika la kiserikali la usafiri wa majijijini Mwanza lijulikanalo kama Marine Service Co. Ltd.

Flaviana Matata ametoa jumla ya vifaa hivyo 500 (vyombo vya kuokoleamaisha ndani ya maji) ikiwa ni kumbukumbu ya kuzama kwa meli ya MvBukoba mnamo Mei 21 mwaka 1996 ambapo pia alimpoteza mama yake mzazi katika ajali hiyo iliyouwa watu takribani 1,000. 

Sababu mojawapo  kubwa iliyofanya watu kupoteza maisha yao siku ya tukio hilo ilikuwa upungufu na ukosefu wa vifaa vya majini kama maboya (Live Vest).

No comments:

Post a Comment